TUICO YAFUNGA MKATABA WA HALI BORA NA SERENGETI

Leo Alhamisi, Aprili 08, 2021 Chama cha Wafanyakazi wa Viwanda, Biashara, Taasisi za Fedha, Huduma na Ushauri (TUICO) kimefunga Mkataba wa Hali Bora kati yake na Kampuni ya Serengeti Breweries Limited (SBL).
Hafla hiyo ya utiaji saini iliyofanyika jijini Dar es Salaam, imeshudiwa na Mwenyekiti wa TUICO Taifa Ndg. Paul Sangeze na Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Waajiri Tanzania (ATE) Dkt. Aggrey Mlimuka.
Katika hafla hiyo, Ndg. Sangeze aliwapongeza viongozi wa pande zote mbili kwa kufanikisha majadiliano ambayo yamepelekea utiaji saini wa makubaliano hayo huku akisisitiza kuendeleza ushirikiano thabiti kati ya Chama na Mwajiri.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa SBL Tanzania Ndg. Mark Ocitti Ongom alifurahishwa na mkataba huo ambapo alisema Serengeti Breweries Limited iko tayari kuusimamia ili kufikia tija, ufanisi kwa mwajiri na waajiriwa sambamba na utatuzi wa changamoto za wafanyakazi.
![]() |
Mkurugenzi
Mtendaji wa Serengeti Breweries Limited Ndg. Mark Ocitti Ongom akisaini mkataba wa hali bora
kati ya TUICO na SBL | Aprili 08, 2021, Dar es Salaam |
Katika hatua nyingine, Mkurugenzi Mtendaji
wa ATE, Dkt. Aggrey Mlimuka alizipongeza pande zote mbili (TUICO na SBL) kwa majadiliano
hayo yenye tija huku akisisitiza kuwa sasa ni muda wa kutumia mkataba huo
kuboresha masilahi ya mwajiri na wafanyakazi.
Dkt. Mlimuka amesema kutokana na utafiti walioufanya kwa vyama vya wafanyakazi nchini, TUICO ni Chama namba moja cha Wafanyakazi katika idadi na ubora wa Mikataba ya Hali Bora hali inayofanya TUICO kuendelea kuwa Chama imara.
![]() |
Mkurugenzi Mtendaji
wa ATE, Dkt. Aggrey Mlimuka akizungumza wakati wa hafla ya utiaji saini mkataba
wa hali bora kati ya TUICO na SBL | Aprili 08, 2021, Dar es Salaam |
Wakati huo huo, Ndg. Tamim Salehe ambaye ni Naibu Katibu
Mkuu wa TUICO na Msemaji Mkuu wa TUICO katika majadiliano hayo, amesema
majadiliano hayo yalianza mwishoni mwa mwaka 2019 na kufikiwa mwezi Februari
2021 ambapo asilimia 75 ya mazungumzo hayo yamefanyika kwa njia ya mtandao
(Zoom Meetings) kutokana na changamoto za Uviko-19.
Pamoja na kuwashukuru wote waliofanikisha zoezi hilo, Ndg.
Tamim aliwakabidhi Wakurugenzi Watendaji kutoka SBL na ATE, Mwenyekiti wa
Majadiliano TUICO-SBL, Mkurugenzi Rasilimali watu SBL, zawadi za sare za Chama
za Sikukuu ya Wafanyakazi Mei Mosi, 2021 na kuwakaribisha katika sherehe hizo
zitakazofanyika kitaifa Jijini Mwanza.
Casino Poker | Play Online With Free Spins No Deposit
ReplyDeleteCasino Poker is one of the most popular online 프리 벳 gambling 마추 자 먹튀 sites. We explain why, if you like to play for 먹튀재판소 fun, you should join 강원랜드 one of our 총판모집
The Wizard of Oz Casino Review, Ratings & Guide (2021)
ReplyDeleteWizard of Oz Casino is powered by 영천 출장샵 Microgaming and boasts a great variety of casino games. The casino also offers a large selection of table games. Rating: 제천 출장마사지 4.7 · Review 안양 출장안마 by 평택 출장샵 Jason Guilbault 울산광역 출장샵